"Hiyo ni Mali Yangu": DP Ruto Amwambia Matiang'i Baada ya Kuanika Utajiri Wake

August 2024 · 2 minute read

Naibu Rais William Ruto amemtaka waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i kufanyia viongozi wote 'Life style audit'.

Akiongea Septemba 2 mtaani Karen alipokutana na wageni kutoka Nakuru, DP alikiri kumiliki mali ambayo ilitajwa na Matiang'i.

Alisema asilimia 70 ya mali hiyo ambayo ni pamoja na helikopta tano na mamia ya ekari ni matunda ya jasho lake.

"Hawa watu wa OP (afisi ya rais) walinisaidia kufanya life style audit, nilikuwa nimefanyiwa na amagazeti hapo awali lakini sasa wametoa ile haikuwa yangu kama hoteli ya 680. Walipata kama 70% hivi ni kweli," alisema DP.

Alitaja hatua ya Matiang'i kama lifestyle audit na kumtaka kuendelea na kuwafanyia viongozi wengine pia.

Pia soma

Magazeti Ijumaa: Matiang'i Apendekeza Ruto Apewe Maafisa 30 Pekee

"Sasa tuendelee hivyo, namna hiyo ... tuambiwe ya ule mwingine na mwingine, hiyo ni sawa," alisema Ruto

Matiang’i aliiambia kamati hiyo kwamba DP anamiliki kituo cha gesi mtaani Kitengela, shamba la Murumbi lenye ekari 395 huko Transmara Narok na lingine la ekari 6,073- ADC Laikipia Mutara Ranch.

Mali zingine zilizoorodheshwa zinazolindwa na maafisa wa polisi ni: Hoteli ya Dolphine, Mombasa (LR. MN / 1/3266) -3 Ekari (6), Shamba la Mata - Taita Taveta (LR. 10287/10 & 11) Ekari 2,537 (6), Makazi yake ya Kibinafsi Elgon View Eldoret (4).

Shamba la Kuku la Koitalel Eldoret (4), makaazi ya Kibinafsi eneo la Kosachei Eldoret (Magereza 3, 1 AP), Kwae Island Development Ltd - Uwanja wa ndege wa Wilson (helikopta 5 za DP).

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZ4F5gJRmn6Kxn2K7qnnMmqOiZamWu6jBjJ2nZqqlqbxurcywmKaamZZ6rq3Topinn5lir6Ktw5pkspldoMKiusikmGatpJa3qr7IZq6ao5VjtbW5yw%3D%3D